Saturday, 30 August 2025

WADAU WA UTALII WAZIDI KUITIKIA WITO WA SERIKALI.

...

-Hoteli ya Kifahari ya Mapito Safari Camp yazinduliwa rasmi Serengeti

Matokeo ya jitihada kubwa za Serikali ya Tanzania kutangaza vivutio pamoja na kuvutia wawekezaji wa kimataifa kuja kuwekeza nchini zinazidi kuzaa matunda kwani alhamisi, Agosti 29, 2025 imezinduliwa hoteli ya Mapito Safari Camp katika kijiji cha Robanda, Serengeti iliyojengwa na kampuni kubwa na maarufu ya hoteli duniani kutoka nchini Marekani ya Marriott.

Dkt. Thereza Mugoba, Mkurugenzi wa Idara ya Utalii Wizara ya Maliasili na Utalii ameshiriki uzinduzi huo akimuwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Hassan Abbasi, hafla hiyo pia pamoja na wageni wengine imehudhuriwa na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania Bw. Andrew Lentz.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger