Na Mwandishi wetu, Arusha
Leo, tarehe 16 Agosti 2025, jijini Arusha, katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC, kumezinduliwa rasmi mafunzo maalum kwa waandishi wa habari na watangazaji yanayolenga maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Mafunzo hayo yamefunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mhe. Kali Salum, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Kenani Kihongosi.
Lengo kuu la mafunzo haya ni kuwaongezea uelewa wanahabari kuhusu weledi, maadili na wajibu wao katika kipindi cha uchaguzi, ili kuhakikisha taarifa sahihi na zenye kuzingatia misingi ya kitaaluma zinawafikia wananchi kwa wakati.











0 comments:
Post a Comment