Sunday 1 March 2020

Raia wawili wa Afrika Kusini Nchini Japan wapata Corona

...
Watu wawili raia wa Afrika Kusini, wafanyakazi katika meli ya ‘Diamond Princess Cruise Ship’ wamekutwa na virusi vya Corona nchini Japan.

Hii ni kesi ya kwanza ya virusi vya Corona kwa wananchi wa Afrika Kusini ndani na nje ya nchi.

Alhamis Februari 27, rais wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa, alitangaza kuwarudisha nyumbani wananchi wote wa Afrika Kusini waliopo Wuhan, China, eneo mlipuko wa virusi hivyo ulipoanzia.

Huku virusi vya Corona vikiendelea kutapakaa sehemu mbalimbali duniani, kwa Afrika Nigeria wiki hii, imerekodi muathirika wa virusi vya Corona ambaye ni raia wa Italia.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger