Tuesday 31 March 2020

Atiwa Mbaroni Kwa Kumfundisha Mbwa Kuendesha Gari

...
Mwanaume mmoja kutoka Lakewood Washington nchini Marekani, amekamatwa kwa kosa la kumfundisha Mbwa wake mwenye jinsia ya kike kuendesha gari kwa spidi, hali iliyopelekea kusababisha ajali.

Jamaa huyo alimuweka Mbwa wake katika siti ya dereva, ambapo amesababisha ajali ya gari mbili zilizokuwa mbele yake bahati nzuri hakukuwa na mtu aliyepata majeraha kwenye ajali hiyo.

Ripoti ya msemaji wa Jeshi la Polisi la Washington State Patrol amesema  "Gari la mtuhumiwa lilikuwa linaendeshwa kwa spidi sana tena isiyo ya kawaida, ameendesha maili 109 kwa muda wa saa moja,na alikuwa anajaribu kutukwepa lakini imeshindikana, tunashukuru baada ya ajali hiyo hakukuwa na mtu yeyote aliyepata majeruhi imekuwa kama miujiza".

Pia  ameendelea kusema tayari wanamshikilia mtuhumiwa huyo kama atataka kuachiwa kwa dhamana itabidi alipe fedha za Kitanzania Shilingi milioni 19, na mbwa wake amehifadhiwa kwenye mazingira ya wanyama wengine baada ya mmiliki wake kukamatwa.

Kwa upande wa mtuhumiwa anayemmiliki mbwa huyo amejitetea kwa kusema, alikuwa anamfundisha  mbwa wake jinsi ya  kuendesha gari.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger