Friday 27 March 2020

KENYA YAANZA KUTEKELEZA AMRI YA WATU KUONDOKA MTAANI KUANZIA SAA MOJA USIKU KUKABILIANA NA CORONA

...
Amri ya kutotoka nje Nchini Kenya kuanzia saa moja usiku hadi saa kumi na moja alfajiri imeanza kutekelezwa mwendo wa saa moja huku huku wafanyakazi wa huduma muhimu pekee wakiruhusiwa kuwa nje usiku hali itakayosaidia kupunguza utangamano baina ya watu na mikusanyiko mikubwa ili kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona.

Serikali ya Kenya imewaonya Wakenya dhidi ya kukiuka amri ya Rais ya kutotoka nje kuanzia mwendo wa saa moja jioni ambapo  maafisa wa polisi watakuwa wakifanya misako mitaani na kuwakamata wananchi watakaokuwa wakirandaranda kuanzia mwendo wa saa moja jioni. 

Mwendo wa saa kumi na mbili Wakenya wengi wameonekana wakiharakisha kuelekea nyumbani hatua iliyosababisha msongamano katika barabara kadhaa huku wale waliokuwa wakitumia magari ya umma wakionekana kusubiri katika vituo vya magari hayo licha ya muda kuyoyoma.

Hata hivyo wengine wao walikata kauli na kuanza kutembea kwa miguu wakihofia kukamatwa na maafisa wa polisi.

Mjini Mombasa na Eldoret mpango huo ulianza kwa mkosi baada ya maafisa wa polisi kukabiliaNa na wakazi saa mbili kabla ya amri hiyo kuanza kutekelezwa.

Katika mtafaruku huo waandishi wa habari pia hawakusazwa huku baadhi yao wakichapwa na polisi kwa kujaribu kurekodi katika kamera zao yaliyokuwa yakijiri.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger