Monday 30 March 2020

Breaking : IDADI YA WAGONJWA WA CORONA TANZANIA YAFIKIA 19

...

 Waziri wa Afya nchini Tanzania, Ummy Mwalimu amesema wagonjwa wa corona nchini Tanzania wamefikia 19, baada ya watano kuongezeka leo Jumatatu Machi 30, 2020.
Taarifa iliyotolewa na waziri huyo leo inaeleza kuwa wagonjwa hao watano walifanyiwa vipimo katika maabara kuu ya Taifa, “kati ya wagonjwa hawa, watatu ni kutoka Dar es Salaam na wawili kutoka Zanzibar ambao taarifa zao zimetolewa na Waziri wa Afya Zanzibar.”

“Hivyo sasa jumla ya wagonjwa wa corona ni 19 akiwemo mgonjwa mmoja aliyetolewa taarifa na Waziri wa Afya Zanzibar Machi 28, 2020.”

Kuhusu taarifa za wagonjwa wapya wa Dar es Salaam, Ummy amesema, “mwanaume mwenye miaka 29 Mtanzania alikutana na raia wa kigeni kutoka miongoni mwa nchi zilizoathirika zaidi. Mwanamke mwenye miaka 21 Mtanzania ambaye ni miongoni mwa watu waliokuwa wakifuatiliwa.”

“Mwanaume mwenye umri wa miaka 49 Mtanzania ambaye pia ni miongoni mwa watu waliokuwa wakifuatiliwa.”




Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger