Monday 30 March 2020

Jiko La Mkaa Lasababishavifo Vya Watu Wanne Shinyanga

...
SALVATORY NTANDU
Wakazi wanne wa kitongoji cha Ngilimba ‘B’ kata ya Ulowa halmashauri ya Ushetu mkoani Shinyanga wamefariki dunia baada ya kuvuta  hewa yenye sumu  iliyosababishwa na mkaa waliouwasha kwenye jiko na kisha kuliweka ndani ya nyumba yao ili kujikinga na baridi.

Akungumza na Waandishi wa Habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba alisema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Machi 28 mwaka huu  ambapo wanafamilia hiyo waligundulika kupoteza Maisha ndani ya nyumba yao wakiwa wamelalala  baada ya kuvuta hewa yenye sumu.

Kamanda Magiligimba aliwataja waliofariki dunia ni pamoja Masanja Emmanuel (35) ambaye ni baba wa familia hiyo,  Mngole Masanja (25) mkewe, Holo Masanja,(05) na Matama Masanja (03) wote wakazi wa Ngilimba.

“Tukio hili limesababishwa na  mvua iliyonyesha Machi 27 iliyoambatana na  baridi kali ndipo marehemu hao waliamua kulala na  jiko la mkaa ndani ya nyumba yao na kusababisha mgandamizo wa hewa kuwa mdogo uliosababisha wavute hewa yenye  sumu ya carbon monoxide”,amesema  Magiligimba.

Miili ya marehemu hao imekabidhiwa ndugu zao kwa ajili ya taratibu za mazishi baada ya kufanyiwa uchunguzi wa daktari.

Mwisho.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger