Friday 27 March 2020

Breaking : AJENTI WA BASI LA KISIBO AFARIKI DUNIA KWA KUKANYAGWA TAIRI AKIDANDIA BASI SHINYANGA

...
Wakala/Ajenti wa Basi la Kisibo Athuman Hamad (38) lenye namba za usajili T192 DBZ linalofanya safari zake kutoka Mwanza kwenda Dar es Salaam amefariki dunia kwa kugongwa na basi hilo wakati basi likitoka katika Stand kuu ya mabasi mkoa wa Shinyanga.

Tukio hilo limetokea leo Ijumaa Machi 26,2020 majira ya saa mbili na dakika 20 asubuhi wakati Wakala huyo akidandia basi hilo na kisha kuanguka na kukanyagwa na basi akafariki dunia hapo hapo.

Mashuhuda waliozungumza na Malunde 1 blog wanasema Athuman Hamad ni Wakala wa Basi la Kisibo alikuwa anatokea Mwanza na basi hilo alipofika Shinyanga alishuka basi lilipoanza kuondoka akawa anakimbilia hilo basi ambalo lilikuwa linatoka getini akadondoka chini akakanyagwa na tairi za basi hilo.

"Huyo Wakala huwa huwa wanasindikiza magari hayo kwa ajili ya kukusanya pesa, walipofika stendi wakasimama kupakia abiria. Wamepakia abiria walipomaliza basi likaanza kuondoka,yeye alikuwa nje ya basi sasa wakati anakimbilia hilo basi ambalo lilikuwa linatoka getini likikata kona,mlango wa basi ukacheza,akadondoka chini akakanyagwa na tairi za basi hilo.
 
Mwili wa marehemu Athuman Hamad ukiwa chini baada ya kukanyagwa na basi

Mwili wa marehemu Athuman Hamad ukiingizwa kwenye gari la polisi

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger