Monday 30 March 2020

Sita wajeruhiwa na fisi Shinyanga

...
Watu sita wa familia moja wakazi wa kijiji cha mwangalanga kata ya Samuye wilayani Shinyanga wamejeruhiwa kwa kung’atwa na fisi katika maeneo mbalimbali ya miili yao na ikidaiwa watu hao wamejeruhiwa na fisi huyo baada ya kumzingira kwa lengo la kumuua

Tukio hilo lilitokea Machi 27, saa 10 jioni, katika kijiji cha Mwangalanga wakati fisi huyo alipovamia kijiji hicho na wananchi kumzingira kwa kumpiga na kusababisha watu hao sita kujeruhiwa.

Taarifa iliyotolewa juzi na Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Deborah Magiligimba, ilisema baada ya watu hao kujeruhiwa walikimbizwa hospitali kupatiwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri.

Aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni Zengo Jitonja, Nkuba Deteba, Juma Salaganda, Limbu Mihambo, Dutu Mdese, na John Matanda.

"Watu hawa wakati wakiwa wamemzingira fisi huyo na kuanza kumshambulia, aliwang'ata sehemu mbalimbali za miili yao, majeruhi watano walipata majeraha madogo na wemeruhusiwa kutoka hospitali," alisema Magiligimba.

"Majeruhi mmoja Nzengo Jintonja, ambaye alijeruhiwa vibaya kwa kung'atwa mikononi na mdomoni, yeye alikimbizwa na kulazwa katika Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Shinyanga na hali yake siyo mbaya sana," aliongeza.

Alisema fisi huyo ameshauawa na wananchi walioendelea kumshambulia kwa kumpiga.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger