Thursday, 9 May 2019

CHADEMA YATISHIA KUTOA TAARIFA YA KUTEKWA MDUDE POLISI WAKINYAMAZA

...

 Chadema imelitaka Jeshi la Polisi kueleza kilichomtokea Mdude Nyagali maarufu Mdude Chadema aliyepatikana jana usiku baada ya kutekwa kwa siku tano.

Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itikadi, Uenezi na Mambo ya Nje wa chama hicho, John Mrema amesema leo, Mei 9, 2019 kuwa polisi isipotoa taarifa hiyo mapema, Chadema wataeleza.

Mrema amesema kwa sasa hawataki kuingilia kazi ya polisi kwani wanaamini watafanya kwa uadilifu, lakini ni muhimu wakaueleza umma kinachoendelea.

“Wameshamhoji Mdude na tuna taarifa kuwa katika uchunguzi wao kuna watu wengine kule Songwe wamehojiwa, basi waondoe hii taharuki kwa kuweka wazi angalau kidogo kuhusu suala hili,” amesema Mrema.

Amesema, “wakishindwa kufanya hivyo kwa haraka, basi sisi hatutanyamaza tutaweka wazi kile ambacho Mdude aliwaambia polisi maana wakati anahojiwa viongozi wa chama walikuwepo.”
Na Elizabeth Edward, Mwananchi 

Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger