Thursday 30 May 2019

KAMPUNI YA JATU KUFANYA MKUTANO MKUU WA WANAHISA WAKE JUMAMOSI,JUNI MOSI JIJINI DAR

...

Mkurugenzi  Mtendaji wa JATU  PLC  Peter Isare
***
Mkutano mkuu wa Kampuni ya Umma ya Jenga Afya, Teketeza Umaskini (Jatu TLC) umepangwa kufanyika Jumamosi June Mosi, katika Ukumbi wa Mgulani jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, wanachama wa Kampuni hiyo watachagua viongozi wapya wa bodi ambao watakua na jukumu la kuingiza kampuni hiyo kwenye soko la hisa ( DSE)

Mkurugenzi  Mtendaji wa JATU  PLC  Peter Isare alisema kuwa kampuni hiyo itaingia rasmi kwenye soko la hisa mapema mwezi August kwa mtaji wa Shilingi Bilion 7.5

Akizungumzia kampuni hiyo alisema ilianzishwa na vijana 2015 kuhusiana na masuala ya afya na lishe na haki za binadamu, watu wengi wanapata changamoto kwenye masuala mbali mbali, "Wengi ni maskini wanashindwa kumudu gharama za maisha na kusababisha migogoro kwenye jamii,"alisema na kuongeza

"Tuwe na afya lakini tuweze kujitegemea na kuwa na afya nzuri, tumejikita kwenye kilimo, masoko na bima ya afya, watu wengi wanahitaji kuwekeza katika biashara na kuhitaji mikopo.

Alisema kampuni hiyo ya umma imesajiliwa mwaka 2016 na imefanikiwa katika Kilimo cha Mpunga Kilombero, Manyara kilimo cha Alizeti na Mahindi, Tanga kulimo cha Maharage.

"Tunawawezesha wakulima kulima kilimo cha kisasa, na kuwapatia wataalamu ambao watawapa elimu, na kilimo ni cha muda wote kisichotegemea hali ya hewa.

"Igima kiwanda cha kukoboa mchele, Kibaigwa kiwanda cha mahindi na alizeti, tunaunganisha kilimo na viwanda, na soko tumelitengeneza wenyewe."

Alisema Jatu unaponunua chochote kama chakula, ni rahisi kukuza faida Kwani kuna mfumo rasmi wa kugawa faida, mteja akinunua bidhaa anapata bonasi ambapo gawio analipata mwisho wa mwezi.

Alisema kampuni hiyo imekuwa inawawezesha wakulima kulima kilimo cha kisasa, na kuwapatia wataalamu ambao wanawapa elimu, na kilimo ni cha muda wote kisichotegemea hali ya hewa.

“Kilimo kinalipa ukikitilia manani, Jatu tuna watu zaidi ya 13,000 ambao wanafanya kilimo na biashara, kama kampuni tunanufaika pia na kupata mazao moja kwa moja kutoka kwa mkulima bila kupitia kwa madalali wa kati.” alisema 


Alisemaunaweza kujiunga kwa kuuza bidhaa upata mgao kila mwezi au ujiunge kwenye kilimo, au kununua hisa kupata gawiwo ukapata faida kutokana na faida ya kampuni.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger