MSANII wa filamu Bongo, Miriamu Jolwa ‘Jini Kabula’ amefunguka kuwa hayupo tayari kuzaa tena nje ya ndoa mpaka atakapoolewa.
Msanii wa filamu Bongo, Miriamu Jolwa ‘Jini Kabula’.
Akistorisha na paparazi wetu, Jini Kabula alisema hawezi kurudia tena
jambo hilo kwani anaogopa kuchanganya damu kwa vile baadaye watoto
wanaweza kuja kugombana na kukosa maelewano hivyo anamuomba Mungu
atimize ahadi ya kuolewa ndipo azae. “Nilizaa
na Chuz kwa sababu tulikubaliana kuzaa tu na siyo kuoana hivyo kwa sasa
nasubiri niingie kwenye ndoa ndipo nizae, sitaki kuwachanganya watoto
wangu,”alisema Jini Kabula.
0 comments:
Post a Comment