Monday 26 May 2014

Safari ya Uturuki yamfanya King Majuto aandae filamu iitwayo Strange of Turkish

...
Baada ya kutembelea nchini Uturuki, msanii wa vichekesho nchini, King Majuto ameanza kuandaa filamu yake mpya iitwayo ‘Strange of Turkish’ itakayohusisha tamaduni ya Tanzania na Uturuki.
10299849_553698514750727_644076135_n Mzee Majuto, Ray, JB na Irene Uwoya wakiwa nchini Uturuki
Akizungumza na Mtandao wetu, Mzee Majuto amesema kuwa baada ya kuushangaa mji wa Instabul na jinsi wanavyozitumia tamaduni zao kwenye maisha ameona aandae filamu itakayoonyesha maisha hayo.

“Nimefanya kazi, sio tu na wasanii wa Uturuki pia kuna Watanzania ambao wanaishi kule, nimejifunza vitu vingi sana, wenzetu wanathamini vya kwao,” amesema. “Nimeshangaa kuona treni za chini,Uturuki umeme haukatiki hata siku moja, yaani kule hakuna kitu kinashindikana kwao. Kwahiyo kutokana na hali hiyo ikanijia wazo nifanye kitu, Strange of Turkish. Filamu na vipande vya Uturuki nimeshashoot, bado huku Tanzania, ni filamu yangu mwenyewe.”
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger