Wednesday 28 May 2014

MASTAA WAONESHANA JEURI YA FEDHA

...
FEDHA inaongea! Mastaa wanaowakilisha Klabu ya Bongo Movie Unity na Shirikisho la Filamu Nchini (TAFF) wameonesha jeuri ya fedha kwa kuwatunza maharusi, mwigizaji Vanita Omary na mumewe Paul Mtenda.
Mastaa wa Bongo Movies wakionyesha jeuri ya fedha katika harusi ya msanii Vanita Omary na mumewe Paul Mtenda.
Sherehe hiyo ilifanyika Jumamosi iliyopita katika Ukumbi wa Mwika, Sinza jijini Dar ambapo pamoja na zawadi nyingine, maharusi hao waliondoka na shilingi millioni tatu, fedha taslimu.
Mpango mzima wa kuwamwaga ‘minoti’ uliongozwa na muigizaji Yobnesh Yusuf ‘Batuli’, Mwenyekiti wa Bongo Movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’, Jacob Steven ‘JB’, Kulwa Kikumba ‘Dude’ na wengineo ambapo mwishoni hesabu ya jumla ilitimia shilingi milioni tatu.
Mwenyekiti wa Bongo Movies, Steve Nyerere akisherehesha katika harusi hiyo.
Kwenye sherehe hiyo, hawakuonesha utengano, hawakujali kama ni memba wa Bongo Movie au Shirikisho la Filamu Nchini (TAFF) lililowakilishwa na rais wake, Simon Mwakifamba ambaye muda wote alionekana mwenye furaha.
Paul Mtenda akiwa na 'mai waifu wake' Vanitha.
Mbali na Steve Nyerere, JB, Batuli na Dude, mastaa wengine waliohudhuria sherehe hiyo ni pamoja na Issa Mussa ’Cloud 112’, Elizabeth Michael ‘Lulu’, William Mtitu, Single Mtambalike ‘Rich’, Yvonney Cherry ‘Monalisa’, Suzan Lewis ‘Natasha’ na wengine wengi.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger