Friday 30 May 2014

MAMBO 6 AMBAYO WANAUME HAWAPENDI KUFANYIWA NA MADEMU ZAO

...



Haya niliyapata kutoka kwa mshauri wa masuala ya mahusiano, ndoa na vijana Frederick Kyara. Hizi ni baadhi tu nakuwekea hapa japo kuna vitu pia wanawake hawavipendi kutoka kwa wenzi wao wanaume. Nayo ni haya hapa, ungana nami kujadili jambo hili ambalo kwangu nimeona ni changamoto au niseme sikujua. 

1. Wanaume hawapendi kuambiwa cha kufanya na wenzi waoMwanamke unapotaka mwanaume afanye jambo usimwambie alifanye bali fanya kama una mpa ushauri. Kwamba John hivi kwa nini tusiweke balbu hapa kwenye korido maana kuna giza kweli. Badala ya hivi wewe John huoni hapa kwenye korido kuna giza balbu imeungua mwezi sasa hujabadilisha kwa nini? Weka balbu bwana. Atafanya au asifanye kabisa kwa sababu umemwambia cha kufanya. 

2. Wanaume hawapendi mwenzi mwenye makelele, mlalamishiYeye ni kulalamika kuanzia Jumatatu hadi Jumapili. Japo wanawake nao wanasema kuna wanaume walalamishii balaaa. Na wenye gubu wanasusa kula mpaka kuongea wanawanunia wake zao mmmmh!

 3. Wanaume hawapendi mwenzi mchafu Mchafu wa mwili wake na hata nyumbani kwenye suala la kutunza nyumba wanayoishi. Uchafu hufanya mwanamke apoteze mvuto. 

4. Wanaume hawapendi mwenzi mbishi Japo na wanawake wanasema wanaume ndio wabishi zaidi. Utampa mwanaume ushauri lakini haufanyii kazi ubishi mwingi.


 5. Wanaume hawapendi kuamrishwa na mwenzi wao Mwenzi mbabe anaetoa amri na kumtawala hawataki.

 6. Wanaume hawapendi kuhisiwa hisiwa na kusachiwa sachiwaKumpekua kwenye simu, mifuko ya suruali kwamba unamulika mwizi. Hawapendi, tena pengine hawajafanya jambo la kuwafanya wahisiwe vibaya.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger