Friday 30 May 2014

KIMENUKA BONGO MOVIE!!..STEVE NYERERE, BABA HAJI WATAKA KUZICHAPA MSIBANI

...

MAJANGA! Mwenyekiti wa Klabu ya Bongo Movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na muigizaji Adam Haji ‘Baba Haji’ nusura wazichape baada ya kupishana kauli.

Mwenyekiti  wa Bongo Muvi, 'Steve Nyerere' (aliyeshika chupa ya maji) akilia kwa uchungu katika msiba wa Recho.
‘Uwanja wa vita’ ulikuwa ni kwenye msiba wa mwigizaji mwenzao Sheila Haule ‘Recho’, Sinza-Palestina, jijini Dar ambapo chanzo kilishuhudia mtiti huo, kilidai tatizo liliibuka mara baada ya Steve Nyerere kumchimba mkwara Baba Haji asijiweke karibu na Jacob Steven ‘JB’.
Muigizaji mkongwe wa Bongo Muvi, Adam Haji ‘Baba Haji’ (kushoto) akishiriki kubeba jeneza lenye mwili wa marehemu Recho.
“Hata haikujulikana kwa nini Steve hakutaka Baba Haji awe karibu na JB, akammaindi ndipo mtiti ulipoibuka, wakataka kushikana mashati bahati nzuri Mtitu (William) akawaamua,” kilieleza chanzo.
Akizungumzia sakata hilo baada ya kutulizwa ‘munkari’, Baba Haji alisema anamshangaa Steve kwa kumchimba mkwara asikae na JB pasipo kuwa na sababu za msingi.
“Sijui jamaa vipi, au ananionea wivu, nashindwa kumuelewa,” alisema Baba Haji huku Steve akichomoa kuzungumza lolote.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger