Friday 23 May 2014

PAMOJA NA MBWEMBWE NYINGI... TICHA AVUNJA NDOA YA MTU

...




RB namba STK//RB/4457/2014 -KUTUMIA LUGHA YA MATUSI inawahusu wanandoa waliodumu kwa zaidi ya miaka 10, waliofunga ndoa kwa mbwembwe nyingi, Nyange na Ruth kisa kikielezwa kuwa ni ticha anayedaiwa kuvunja utatu huo mtakatifu, Ijumaa lina kisa na mkasa.

PAMOJA NA MBWEMBWE NYINGI... TICHA AVUNJA NDOA YA MTU


RB namba STK//RB/4457/2014 -KUTUMIA LUGHA YA MATUSI inawahusu wanandoa waliodumu kwa zaidi ya miaka 10, waliofunga ndoa kwa mbwembwe nyingi, Nyange na Ruth kisa kikielezwa kuwa ni ticha anayedaiwa kuvunja utatu huo mtakatifu, Ijumaa lina kisa na mkasa.
Ruth na Nyange wakati wa harusi.
Habari zilieleza kwamba wahusika ni  wakazi wa Pugu, Dar.

Kwa mujibu wa habari za mtaani wanakoishi wawili hao wanadaiwa kufikishana kwenye Kituo cha Polisi cha Sitaki-Shari, Dar baada ya mke  kumfungulia…
Stori: Haruni Sanchawa
RB namba STK//RB/4457/2014 -KUTUMIA LUGHA YA MATUSI inawahusu wanandoa waliodumu kwa zaidi ya miaka 10, waliofunga ndoa kwa mbwembwe nyingi, Nyange na Ruth kisa kikielezwa kuwa ni ticha anayedaiwa kuvunja utatu huo mtakatifu, Ijumaa lina kisa na mkasa.
Ruth na Nyange wakati wa harusi.
Habari zilieleza kwamba wahusika ni  wakazi wa Pugu, Dar.
Kwa mujibu wa habari za mtaani wanakoishi wawili hao wanadaiwa kufikishana kwenye Kituo cha Polisi cha Sitaki-Shari, Dar baada ya mke  kumfungulia mumewe jalada hilo la kesi baada ya ndoa yao kupigwa kimbunga.
Kuna madai mazito kwamba mke anamlalamikia mumewe kumjali zaidi hawara ambaye anadaiwa naye ni mke wa mtu akiwa ni mtumishi wa serikali yaani mwalimu.
Akisimulia kila kitu kwa gazeti hili, Ruth aliyefukuzwa na mumewe alisema kwamba utatu wake na mumewe uliingia mchanga kitambo bila yeye kujua chanzo kwani hakuwa mfuatiliaji lakini baada ya kufuatilia alibaini kuwa kuna mchepuko kwenye ndoa yake.
Ruth na Nyange wakiwa wenye furaha wakati wa ndoa yao.
“Nilikuwa sijui ndoa yangu  inachezewa na mtu gani, baadaye nilinasa mawasiliano ya simu ilibidi  nifanye uchunguzi wa kina  ili kumbaini mbaya  wangu kitu ambacho nilikifanikisha kwa  kiasi  kikubwa alisema Ruth.
Kutokana  na hali hiyo mume wake aliendelea  kufanya manyanyaso huku  akiendelea na mawasilino ya karibu  na   mwalimu huyo ambaye pia ni mke wa  mtu.
Mama huyo alidai kuwa mume wake amekuwa na mahusiano ya kimapenzi  na mke wa mtu huyo ambaye ni huyo  mwalimu na kusababisha pia ndoa yake kuingia matatani.
Ninachokizungumza ni sahihi kwa  sababu hata siku ninamkamata  mume  wangu alikuwa kwa mwalimu huyo ambapo siku hiyo alimpelekea  sukari na matumizi mengine hali  iliyosababisha timbwili kubwa,  nilifanikiwa kumnyang’anya  mume wangu  ile mizigo aliyokuwa  amepeleka kwa huyo mwanamke.
Mpaka sasa tunavyoongea huyo mwalimu ndoa yake iko matatani  kutokana na jeuri aliyokuwa akipewa  na mume wangu maana inadaiwa  kuwa hata nyumba anayoishi mume  wangu ndiye mlipa kodi.
Katika kikao kilichokaa shuleni  mwaka jana kwa mwalimu huyo  kuhusiana na tukio hilo, mwalimu huyo alikiri kuwa na mahusiano na mume  wangu lakini aliahidi kuachana naye  mbele ya kikao hicho, cha kushangaza hadi leo bado wanaendelea na mahusiano.
Alipoulizwa mwalimu huyo ambaye  ametajwa kwa jina moja la Catherine  Rokio Mayengo au Elizabeth Rokio Mayengo kwa  njia ya simu kuhusiana  na sakata hilo alimwambia  mwandishi  wetu kuwa  namuuliza kama nani.
Mwandishi alijitambulisha na kumwambia anataka kujua hayo  yanayosemwa na Ruth Nyange mwalimu yana ukweli gani.
Mwalimu huyo alisema hawezi  kuongea na udaku  hivyo kama ni  kuandikwa habari hiyo iandikwa kadiri mwandishi anavyoweza.
Mbali na hilo mwalimu huyo alimwandikia ujumbe mwandishi wetu unaosema kuwa yeye anamilikiwa na serikali na haogopi kitu au jambo lolote na anajiamini na anapenda watu  wanaotumwa kama mwandishi waende Stakishari.
Mwandishi wetu alifanikiwa kumpata  mume wa mwalimu huyo ambaye  alijitambulisha kwa jina la Evansi na kukiri kuwa huyo ni mke wake wa ndoa lakini hawako naye kwa muda huu.
Kuhusu mke wake kuwa na uhusiano na mtu mwingie, alisema inawezekana  maana alianza ukorofi na kuamua kwenda kupanga lakini taarifa zilizopo  amepangishiwa na mwanaume  ambaye yeye hamjui.
Huyo mwalimu ni mke wangu wa  ndoa hata mimi ninashangaa kuacha  ndoa yake na kwenda kupanga na  kuacha watoto wawili ambao tumezaa  wote wakiwa wanateseka kwa kukosa mapenzi ya mama.    
Mwandishi wa habari hii alifanya kila  mbinu ya kukutana na mlalamikiwa  ambaye ni Grey Godwin Nyange lakini  ilishindikana na kujibu kwa njia ya simu kuwa habari anazoambiwa  hazifahamu labda huyo aliysema hayo ndiye anayejua undani wake.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger