
Katika tukio hilo mama yake Mueni aliyetambulika kwa jina la Monica Matolo, 75, alipata majeraha kadhaa ya moto na kukimbizwa hospitali ya rufaa ya Makueni kwa ajili ya matibabu.
Aidha, katika uokozi huo mali za thamani zilishindwa kuokolewa na zikateketea. Taarifa zinaeleza kuwa nyumba hiyo ilikuwa na harufu kali ya petroli jambo linaloonyesha kuwa kuna mtu alihusika kuunguza nyumba hiyo.
Polisi wanamhisi kaka yake Mueni kuhusika katika tukio hilo kutokana na kuwapo kwa mgogoro wa ardhi wa kifamilia. Aidha, miili minne iliyokutwa katika tukio hilo ilibebwa na kwenda kuhifadhiwa mochwari ya hospitali ya rufaa ya Makueni.
0 comments:
Post a Comment