Thursday 28 November 2019

Marekani Yawaunga mkono waandamanji Hong Kong, China Yatishia Kulipiza Kisasi

...
Rais wa Marekani Donald Trump amesaini muswada wa kuunga mkono vuguvugu la maandamano ya kudai demokrasia mjini Hong Kong na kuwa sheria licha ya pingamizi kutoka kwa serikali ya China. 

Sheria hiyo ambayo iliungwa mkono kwa sauti moja bungeni, inahitaji Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani kuthibitisha angalau kila mwaka kwamba uhuru wa Hong Kong haukutatizwa. 

Bunge la Marekani pia limepitisha muswada wa pili - ambao Rais Trump pia ameusaini - unaopiga marufuku usafirishaji na uuzaji wa silaha za kudhibiti maandamano ya umma kwa vikosi vya usalama vya Hong Kong kama vile, mabomu ya kutoa machozi, dawa ya pilipili, risasi za mpira pamoja na bunduki za kutoa mshtuko wa umeme. 

China ilimuonya Trump wiki iliyopita kuwa itachukua hatua za kulipiza kisasi iwapo atasaini miswada hiyo na kuwa sheria.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger