Friday 29 November 2019

Diamond Platnumz Ambwaga Ali Kiba

...
Shirika la Utangazaji CNN limetaja wanamuziki bora 10 barani Afrika, akiwemo msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz.

Orodha hiyo inamfanya Diamond kuwa msanii pekee kutoka Afrika Mashariki kuingia katika orodha hiyo ya wasanii wanaofanya vizuri katika muziki.

Wengine waliotajwa ni Burna Boy wa Nigeria ambaye pia ameteuliwa katika tuzo za Grammy zitakazofanyika Januari 2020 pamoja na Yemi Alade, Tiwa Savage na Wizkid wote wa nchi hiyo.

Mtunzi, mwanaharakati na mshindi wa tuzo ya Grammy kutoka nchini Benin, Angelique Kidjo pia amejumuishwa katika orodha hiyo.

Pia wapo waimbaji wa Afrika Kusini, Sho Madjozi, Busiswa Gqulu ambaye pia ni mwandishi wa nyimbo na mshairi, rapa wa Zambia, Mwila Musonda maarufu Slapdee.

Diamond ambaye ameingia katika tasnia ya muziki miaka 10 iliyopita amekuwa na mafanikio makubwa.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger