Saturday 30 November 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila aagiza mawakala mashine za EFD kukamatwa

...
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila ameagiza mawakala wa mashine za kutoa risiti za kielektroniki (EFD) mkoani humo, kukamatwa na kuwekwa ndani kutokana na kutohudhuria mkutano wa wafanyabiashara soko la Sido, jijini Mbeya leo Novemba 30, 2019.

Chalamila ametoa agizo hilo leo Jumamosi  katika mkutano wake na wafanyabiashara wa soko hilo kwa ajili ya kusikiliza kero zao.

"RPC  watafute leo Jumamosi wapumzike mahali tutakutana nao Jumatatu, haiwezekani huu ni upuuzi tunawahitaji wao hawapo hata sisi tumeacha usingizi," amesema.

Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania mkoani Mbeya (TRA),  Jiji la Mbeya lina mawakala wanne kwa sasa ambao walitakiwa kuhudhuria mkutano huo.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger