Sunday, 5 May 2019

Hizi Ndizo Sehemu utakazopita mwili wa Dr. Mengi Kesho

...
Ratiba ya kuupokea mwili wa Dr. Reginald Mengi, Uwanja wa Ndege wa Mwl. Julius Kambarage Nyerere imeelezwa kuwa itafanyika kesho, Jumatatu, saa 8:00 mchana.

Mwili wake utaletwa na ndege ya Shirika la Ndege la Emirates kutokea Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (U.A.E).

Baada ya mwili kupokelewa katika Uwanja wa Ndege wa JNIA, utapitishwa maeneo ya Tazara, Buguruni, Ilala, Kigogo, Magomeni hadi Kinondoni.

Kutoka Kinondoni, mwili wake pia utapitishwa hadi katika maeneo ya Morocco, barabara ya Bagamoyo, Sayansi, Mwenge hadi katika hospitali ya Lugalo ambako mwili wa Dr. Reginald Mengi utahifadhiwa.

Ratiba hiyo itaendelea siku ya Jumanne ya Mei 7, 2019, ambapo mwili utapelekwa katika ukumbi wa Karimjee, kwaajili ya watu wote kuuaga na kisha utarejeshwa nyumbani kwake. Siku ya Jumatano mwili utasafirishwa kupelekwa Moshi Machame ambako Ibada ya mazishi itafanyika siku ya Alhamis katika kanisa la Kisereni (KKKT).


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger