Saturday, 4 May 2019

Boeing 737 Yashindwa kutua na kuishia kuingia mtoni nchini Marekani.

...
Ndege aina ya Boeing 737 imeshindwa kutua na kuishia kuingia mtoni nchini Marekani.

Hiyo ni aina ile ile ya ndege iliyopata ajali na kusababisha vifo vya mamia ya watu nchini Ethiopia na Indonesia.

Kwa mujibu wa habari,ndege hiyo ilitoka katika barabara yake na kuingia mtoni wakati ikitaka kutua Florida nchini Marekani.

Tukio hilo limetokea katika uwanja wa ndege wa Jacksonville,ambapo ndege hiyo ya abiria iliyokuwa imebeba abiria 136 ilishindwa kutua na mwisho kuingia katika mto wa St.John.

Hata hivyo hakuna aliyeripotiwa kupoteza maisha. Watu wawili wamejeruhiwa.



Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger