Thursday, 9 May 2019

BOBI WINE, BESIGYE WATENGENEZA JEMBE MOJA LA KUMLIMIA MUSEVENI

...

Mbunge wa upinzani nchini Uganda ambaye pia ni msanii wa muziki, Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine, ameungana na mwanaharakati wa kisiasa Dkt. Kizza Besigye ili kukiondoa madarakani chama tawala cha National Resistance Movement (NRM) kinachoongozwa na Rais Yoweri Museveni.

Taarifa iliyotolewa na wapinzani hao wenye nguvu zaidi nchini Uganda, imeeleza kuwa baada ya mazungumzo kati yao, wamekubaliana kuhusu masuala kadhaa ya kushirikiana kisiasa dhidi ya Museveni kwenye uchaguzi mkuu ujao mwaka 2021.

Akizungumza na waandishi habari jana, Bobi Wine alisema wamekuwa wakishauriana katika mikutano kadhaa na vyama tofuati vya kisiasa nchini kikiwemo cha Democratic Party maarufu DP na kiongozi wa People’s Government, Dkt. Kizza Besigye.

Bobi ambaye hana chama, ni mgombea huru na kwa sasa ni Mbunge wa Jimbo la Kyadondo,

NRM kimekuwa madarakani tangu 1986.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger