Wednesday, 17 April 2019

Jela Miaka Miwili Kwa kosa la kughushi na kutumia vyeti bandia.

...
Mahakama  ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Pwani imemuhukumu kwenda jela miaka miwili Anna Kasanda kwa kosa la kughushi na kutumia vyeti bandia.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Rose Kangwa, alisema mahakama imeridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa utetezi kuwa mtuhumiwa alikuwa anatumia vyeti bandia.

“Mtuhumiwa anahukumiwa kwenda jela miaka miwili kwa kosa la kwanza la kughushi leseni ya uuguzi na ukunga kinyume cha kifungu cha sheria namba 355(a) na 337 cha mwaka 2002,” alisema Rose.

Alisema kwa kosa la kujaribu kuihuisha (renew) leseni hiyo, mtuhumiwa atatumikia miaka miwili mingine. 

Rose alisema japokuwa hakuna sehemu katika ushahidi inaonesha mtuhumiwa anamiliki mashine ya kuchapa nyaraka hizo, lakini kwa mujibu wa shahidi wa pili inaonesha kuwa mtuhumiwa alitaka kuendelea kutumia vyeti hivyo.


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger