Monday 29 April 2019

POLISI KUKAMATA WANAOTEMBEA WAMELEWA POMBE MTAANI

...
Polisi nchini Uganda inapania kuzindua mpango wa kuwakamata watembea kwa miguu watakaopatikana wakiwa walevi.

Akitetea mpango huo mpya kamanda wa trafiki katika jiji la Kampala Lawrence Niwabiine amesema kikosi cha polisi hakitaruhusu watu "wahatarishe"maisha yao.

Tayari vyombo vya habari nchini Uganda vimezua gumzo mitandaoni baada ya kuangazia mpango huo tata katika mitandao ya kijamii.

Watu wamekua wakihoji jinsi sheria hiyo itakavyotekelezwa hasa ikizingatiwa kuwa baadhi ya watu wanaokamatwa kila uchao wakiendesha magari wakiwa walevi huishia kuachiwa katika mazingira ya kutatanisha.

Hata hivyo kuna mamia ya watu waliyopatikana na hatia ya kuendesha magari wakiwa walevi wameshindwa kulipa faini.
Hatua hii imepokelewaje?

Gazeti la New Vision limeendeleza gumzo hilo katika mtandao wa kijamii wa Twitter kwa kuelezea sheria hiyo inayopendekeza kuwa mtu akipatikana na hatia atapigwa faini ya hadi dola 10,000 na pia kuwauliza wasomaji wake kutoa maoni kuhusiana na pendekezo hilo.

Kuna wale wanaosema kwa kuwa Afande Niwabiine hatumii kileo huenda maafiasa wake wakawatia mbaroni walevi wanaotembea kwa miguu kando ya barabara.

Wengine wanasema hatua hiyo huenda ikawa na athari kwa uchumi wa nchi.

Wanaharakati wanapendekeza mifumu ya kisheria na kijamii iwekwe sawa kabla ya kuanza kutekeleza sheria hiyo.

''Kabla ya kuanza mpango huo,magereza yatahitaji kupanuliwa haraka iwezekanavyo kwasababu watembezi wengi walevi hawana uwezo wa kulipa faini la sivyo mahakimu watakuwa na kibarua kigumu katika kutoa hukumu dhidi ya watu hao wakati sheria inasem kila mmoja achukukliwe hatua'' alisema mmoja wao.

Pili anasema wafanyibiashara wa pombe watalazimika kuhamisha biashara zao katika maeneo ya makazi ili kupunguza hofu ya wateja wao kukamatwa.

''Hata polisi akipiga kambi karibu na hapo akisubiri kukukamata hataweza kufanya hivyo manake unaweza kuamua kumpigia mmoja wa jamaa zako nyumbani kukuletea mtu ulale ndani ya baa karibu na kwako'' ,aliongeza.

Pia anasema kumbi za burudani zitapoteza umuhimu kwasababu kile ninachowavutia wateja ni pombe

Wafanyibiashara wa texi wapokea vyema pendkezo hilo kwasababu walevi watalazimika kutumia huduma zao za usafiri kwa kuhofia kukamatwa.

Baadhi ya wakaazi wamewaonya wenzo wanaopenda kubugia pombe kuwa makini hata wanapotumia usafiri wa umma kwasababu polisi huenda wakawasubiri katika stendi ya mwisho wa gari.
Chanzo - BBC
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger