Tuesday 30 April 2019

Kiongozi wa IS Abu Bakr al-Baghdad ajitokeza katika kanda ya video baada ya miaka 5

...
Kundi la kigaidi la Islamic State limesambaza mkanda wa video unaodai kumuonyesha kwa mara ya kwanza, baada ya kupita miaka mitano, kiongoza wa kundi hilo Ibrahim as-Samarrai, mashuhuri kama Abubakr al-Baghdadi.

Kundi hilo lilisambaza mkanda huo wa dakika 18 kupitia moja ya mitandao yake ya kijamii hapo jana Jumatatu ambapo kiongozi huyo wa magaidi ameonekana akizungumza na viongozi wengine watatu wa kundi hilo. 

Ukweli wa mkanda huo haukuweza kuthibitishwa mara moja na duru huru. Hata hivyo iwapo kutakuwa na ukweli wowote kwenye mkanda huo, kiongozi huyo wa magaidi atakuwa ameonekana hadhari kwa mara ya kwanza tokea mwaka 2014. 

Mwaka huo gaidi huyo alionekana kwenye mkanda mwingine akitoa hutuba katika moja ya misikiti ya mji wa Mosul, ulioko kaskazini mwa Iraq, akidai kwamba kundi hilo potovu lilikuwa limebuni mamlaka ya ukahlifa katika nchi hiyo na nchi nyingine jirani ya Syria.

As-Samarrai alionekana akizungumza katika mkanda huo wa kwanza baada ya kundi lake la kitakfiri kuteka na kudhibiti maeneo makubwa ya Iraq na Syria ambapo wahanga wengi waliuawa kinyama na kwa namna ya kutisha katika uvamizi huo. 

Licha ya kuwa tarehe ya kurekodiwa mkanda huo wa hivi karibuni haijaweza kuthibitishwa, lakini kiongozi huyo wa magaidi amesikika akizungumzia mashambulio ya kigaidi yaliyotekelezwa hivi karibuni huko Sri Lanka na kupelekea mamia ya watu kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa. 

Kinara huyo wa magaidi wa Daesh( IS) amedai kuwa mashambulio hayo yalitekelezwa na kundi lake kwa shabaha ya kulipiza kisasi cha kushindwa wapiganaji wake katika kijiji cha Baghouz kilichoko mashariki mwa Syria.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger