Wabunge wa kambi ya upinzani wamesema watalihamishia sakata la utata wa Sh.1.5 Trilioni majimboni kwao baada ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhitimisha kuwa fedha hizo hazikuibiwa au kupotea. Uamuzi huo wa wapinzani umetolewa na Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali (CUF). Bobali amesema kuwa ingawa kamati imehitimisha hivyo, wao wataendelea kuwasha moto akidai kuwa fedha hizo zilitumika bila idhini ya Bunge. “Pale tunapohoji ni nani aliyeruhusu fedha hizo zikatumika bila idhini ya Bunge, na ni fedha nyingi. Sasa mjadala ndio kwanza unaanza na ni lazima moto uwake…
0 comments:
Post a Comment