Sakata la ununuzi wa korosho limeendelea kuwasha moto bungeni baada ya Mbunge wa Mchinga (CUF), Hamidu Bobali kusema yupo tayari kujiuzulu ubunge iwapo itathibitika kwamba wakulima hawalipwi Sh2,640 kwa kilo badala ya Sh3,300 iliyotangazwa na Rais John Magufuli. Akichangia taarifa za kamati za Bunge za Bajeti na ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) jana, Bobali alisema kwa taarifa zilizotolewa na Serikali ni wazi kuwa kilo moja ya korosho imeuzwa kwa Sh4,180 na kuitaka kueleza kama itaendelea kuwalipa wakulima korosho daraja la kwanza kwa Sh3,500. “Tunataka kauli kama mmeuza kwa…
0 comments:
Post a Comment