
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo, amewaeleza wanahabari kuwa idadi hiyo inalenga kupunguza changamoto ya upungufu wa walimu shuleni na utoaji wa elimu bora zaidi.
Jaffo alisema ajira hizo zitatangazwa mapema mwaka huu na zitaongeza nguvu kwenye shule zenye uhitaji wa walimu hasa mpya na zile zilizoandikisha wanafunzi wengi wa darasa la kwanza na kidato cha kwanza.
Sambamba na hilo, ameahidi kushirikiana na shule za msingi zilizoandikisha wanafunzi wengi zaidi wa darasa la kwanza ili shule hizo zipate miundombinu ya kutosha kuwahifadhi wanafunzi hao.
Amesema kwa kuanza, serikali imejipanga kuongeza majengo katika shule ya msingi Mbagala Majimatitu ambayo imeandikisha wanafunzi wa darasa la kwanza 1,022, idadi ambayo ni sawa na wanafunzi wa shule moja kuanzia darasa la kwanza hadi la saba.
0 comments:
Post a Comment