Saturday 27 February 2016

RAIS MPYA WA FIFA NI GIANNI INFANTINO

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Gianni Infantino

KATIBU Mkuu wa Shirikisho la Soka barani Ulaya-Uefa, Gianni Infantino amechaguliwa kuwa Rais mpya wa Shirikisho la Soka duniani-Fifa.

Infantino alishinda awamu ya pilii ya uchaguzi huo uliofanyika Uswisi kwa kura 88 kati ya kura 207 akifuatiwa na Sheikh Salman Bin Ebrahim Al Khalifa wa Bahrain aliyepata 85.

Mwanafalme wa Jordan Ali Bin Hussein alipata kura 27 na mgombea kutoka Ufaransa Jerome Champagne alipata kura saba.

Infantino mwenye umri wa miaka 45 anashika nafasi hiyo kumrithi Sepp Blatter aliyesimamishwa kushiriki shughuli zozote za soka kwa miaka minane adhabu ambayo ilipunguzwa kuwa miaka sita pamoja na Rais wa zamani wa Uefa Michel Platini kwa tuhuma za rushwa.

"Ndugu zangu, siwezi kuelezea hasia zangu kwa wakati huu," Infantino alisema wakati akizungumza baada ya kuchaguliwa. "Tutarejesha hadhi na heshima ya Fifa. Watu watatupongeza, watawapongeza ninyi kwa mabadiliko tutakayofanya.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger