Wednesday 24 February 2016

Mnaotarajia Kuoa au Kuolewa Chukueni Tahadhari Hii Mapema Usijejuta

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Ewe mwanaume ukioa mwanamke:

Mrefu, jua kwamba utaoa mwanamke mpenda maendeleo, mchapa kazi na mkarimu ila hawajui mapenzi na ni wavivu kujiweka safi kimazingira.

Mfupi kiasi, jua ya kwamba utaoa mwanamke mchangamfu na mpenda elimu sana ila tu wanapenda mnongono na hawaridhiki.

Mfupi kabisa.Jua ya kwamba utaoa mwanamke msikivu na mcha Mungu ila ni waroho kwa kula na wabishi sana.

Ewe mwanamke ukiolewa na mwanaume:

Mrefu, jua ya kwamba utaolewa na mwanaume mwenye upendo, utu na ubinadamu ila ni wabahili mno na hawapendi kupendeza.

Mfupi kiasi, jua ya kwamba utaolewa na mwanaume mwenye fikra na akili timamu za maendeleo, mbunifu, mcheshi na fundi wa mahaba ila ni wapenda ushirikina sana, wana wivu na wambea sana na mara nyingi hupenda kupiga chabo kwa watu wanaofanya mapenzi.

Mfupi kabisa, jua ya kwamba utaolewa na mwanaume mwaminifu, msikivu, mnyenyekevu ila huwa wepesi wa kujiua, kukata tamaa upesi, wanawivu sana na hawapendi kuoga.
Nawatakieni kila la kheri wale wenye wapenzi na ambao mnajiandaa kuoa au kuoelewa ila zingatia sana tabia hizo hapo juu za huyo unayetegemea kufunga nae pingu za maisha ili usije kutusumbua baadae. Chukueni tahadhari!
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger