Monday 22 February 2016

Shule ya Sekondari Ilboru sasa Kuchuja Wanafunzi

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Kufuatia kutofanya vizuri kitaifa katika mtihani wa kidato cha nne, shule ya sekondari ya watoto wenye vipaji maalumu, IIboru itaanza kuwachuja wanafunzi wasio na uwezo wanaopangiwa kusoma shuleni hapo.
 
Mkuu wa shule hiyo, Julius Shula amesema licha ya Ilboru kuwa ya kwanza kwa shule za Serikali nchini, lakini imebaini upungufu katika upatikanaji wanafunzi.
 
Amesema kuna wanafunzi kutoka shule za binafsi wanaopangiwa IIboru, wamebainika hawana uwezo, hivyo kutilia shaka alama walizopata katika mitihani yao ya kuhitimu darasa la saba.
 
“Tayari tumewapa mitihani waliongia kidato cha kwanza, huwezi amini kuna wanafunzi wanapata alama 0, lakini ukifuatilia matokeo ya kuja hapa wana wastani wa alama zaidi ya 200 sasa hili ni tatizo kubwa,” alisema. 
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger