Thursday 25 February 2016

Ndege Ndogo Yapotea ikiwa na Abiria 23

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Ndege ndogo ya shirika la ndege la tara Airlines iliyokuwa na watu 23 wakiwemo watoto imepota ikiwa maeneo ya usawa wa milima Magharibi mwa Nepal.
Ndege hiyo ilikuwa safarini kutoka Pokhara, Magharibi mwa Mji Mkuu Kathmandu, kwenda Jomsom, eneo ambalo watu wengi wanaoenda kukwea milima ya Himalaya huanza safari yao ya kukwea milima hiyo.
Ripoti zinasema mabaki ya ndege hiyo yamepatikana ingawa hakuna taarifa zozote kuhusu vifo au majeruhi.
Taarifa zaidi zinasema kuwa, Ndege hiyo ilipoteza mawasiliano na maafisa wa udhibiti wa safari za ndege wa Pokhara dakika 18 baada ya kupaa na kwamba hakuna viwanja vya ndege kati ya maeneo hayo mawili.
Maafisa wanasema ndege hiyo ya shirika la Tara Airlines ilikuwa na marubani watatu na abiria 20, mmoja wao raia wa China na mwingine wa Kuwait. Wawili kati ya abiria waliokuwa wamebebwa na ndege hiyo walikuwa watoto.
Tangu mwaka 1949, kumetokea zaidi ya ajali 70 zilizohusisha ndege za kawaida na helikopta, na vifo vya watu 700
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger