
Akizungumza kwa uchungu baba wa mmoja wa watoto waliofanyiwa kitendo hicho, Abdillah Mpacha (pichani), alisema tukio lilitokea Kigezi, Chanika ambapo mtoto wake alikuwa akitokea Madrasa.
Alisema, alipokuwa njiani kuelekea nyumbani alikutana na mbakaji huyo na kumlaghai kwa pipi na kashata kisha kumpeleka nyumbani kwake na kumfanyia kitendo hicho.
“Tulipompeleka hospitalini, baada ya uchunguzi na vipimo alionekana kuwa ameharibiwa vibaya sehemu za siri, hapo ndipo akasema ukweli na kumtaja mbakaji akasema alificha kwa sababu alimwambia kama angesema angemchinja.”
Awali tukio hilo liliripotiwa kwenye Kituo cha Polisi Chanika na kufungiliwa jalada namba CHK/RB/718/2014 kabla ya kuhamishiwa Kituo cha Polisi Stakishari na kufunguliwa jalada namba STK/RB/3609/2014 KUBAKA.
0 comments:
Post a Comment