Tuesday 13 May 2014

BREAKING NEWS:KIDATO CHA SITA WOTE MNAKUMBUSHWA KUOMBA MKOPO KABLA YA KWENDA JESHI(JKT)

...

Mojawapo ya eneo linalolalamikiwa  na wanafunzi wa vyuo na taasisi za elimu ya juu kuhusu Bodi ya Mikopo ( HESLB), ni eneo la madaraja wanayopangiwa na bodi hiyo kwa ajili ya kupata mkopo wa  masomo ya kozi wanazochukua.

Kuna malalamiko kwamba, bodi ya mikopo imekuwa ikipanga madaraja kwa upendeleo kwa kuwa ile dhana ya kumkopesha mwanafunzi anayetoka katika familia maskini kwa kiwango cha asilimia 100,haionekani kufanya kazi kwa wanafunzi walio wengi.
Kwa muda mrefu kumekuwa na malalamiko  kwamba,katika upangaji wa madaraja unaofanywa na bodi,wanafunzi wanaotoka katika familia zenye uwezo mkubwa au wa kati, ndio wamekuwa wakipata asilimia 100 na wale wanaotoka katika familia maskini wakiishia kuambulia asilimia 60 mpaka 40. 
April mwaka huu, bodi ya mikopo nchini ilianzisha  utaratibu mpya wa kuomba mikopo kwa wanafunzi wapya na wale wanaoendelea kwa njia ya mtandao.
Mfumo huu unatarajiwa  kuchukua nafasi ya ule wa zamani, ambapo mhusika alikuwa anatakiwa kujaza fomu  kisha kuziwasilisha HESLB. 
Fomu hizo zilijazwa taarifa mbalimbali za muombaji zilizokuwa zinahitajika na bodi ili ziisaidie kumpangia muombaji daraja la fedha alizostahili kupewa kama mkopo kwa ajili ya kulipia gharama mbalimbali anazopaswa atika chuo au taasisi aliyokuwa anachukua kozi yake.

Wanafunzi wote wakidato cha sita mnatakiwa kuomba mkopo kwa kutumia utaratibu wa kulipia MPESA kabla ya kwenda jeshi kuepuka usumbufu.
KWA MAELEZO ZAIDI TEMBELEA :www.heslb.go.tz au olas.heslb.go.tz 
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger