Monday 18 September 2023

TAASISI YA OMUKA HUB YAFUNGUA MKUTANO KUANGAZIA SUALA UKATILI WA KIJINSIA MTANDAONI KWA WANAWAKE KATIKA SIASA

...

Taasisi ya OMUKA HUB ambayo imejikita katika masuala ya maendeleo na ujumuishi wa kidijitali ikiwemo kuhamasisha matumizi ya mtandao kwa wanawake katika siasa, imefungua mkutano wake jijini Dar es Salaam wenye lengo la kuangazia suala la ukatili wa kijinsia mtandaoni kwa wanawake katika siasa.

Akizungumza katika hafla hiyo leo Septemba 18,2023 Jijini Dar es Salaam, Mwanzilishi wa Taasisi hiyo Mhe.Neema Lugangila amesema ukatili wa kijinsia katika siasa una shabiana na ukatili wa wanawake katika habari.

"Tumekuwa na majidiliano mazuri ya namna gani tunaweza kuimarisha uwakilishi na ushiriki wa wanawake katika siasa za mtandaoni na tumekubalina tutaandaa kamati ambayo itaenda kudadavua suala hili ili tuje na mpango kazi ambao tutakapo kwenda kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu wanawake wataweza kushirik katika mitandao ya kijamii kunadi sera zao bila bughudha". Amesema.

Amesema anaelewa kadhia ambayo wanapitia wanawake wanasiasa katika mitandao hivyo wao kama wabunge wanawake wameamua kubeba ajenda hiyo kusemea wanawake katika siasa lwasababu wanatambua umuhimu wa kushiriki katika mitandao

"Sasa kwa kushirikiana na wanawake katika vyombo vya habari tunaamini tunaweza kushirikiana. vzuri na kupaza sauti kubwa ili kuweka mazingira sawia na wezeshi ili wanawake katika siasa waweze kushiriki ipasavyo katika mitandao ya kijamii".Amesema

Kwa upande wake Msemaji Mkuu wa Serikali Mhe.Gerson Msigwa amesema ukatili haukubaliki uwe wa kwenye vyombo vya habari, bungeni au mahali pengine popote hivyo serikali imekuwa ikishiriana na wadau kuhakikisha kwamba kunakua na kampeni mbalimbali za kukabiliana na ukatili dhidi ya wanawake.

Aidha amesema kuwa zipo sheria mbalimbali ambazo vitendo vyote vya ukatili havikubaliki na ni makosa kwa mujibu wa sheria hivyo wanaangalia kama wanaweza kuja na uwanja mpana zaidi wa kisheria wa kukabiliana na hayo majukumu.

Pamoja na hayo amempongeza Rais Samia Suluhu kuwa mstari wa mbele kuhakikisha anaongoza mapambano dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake katika maeneo mbalimbali na kuwawezesha wanawake wenyewe.

"Rais Samia ameandaa Wizara Maalumu ya kukabiliana na vitendo hivi ambayo ni Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, ambapo moja ya kazi ya Wizara hii ni kutoa Elimu kwa jamii juu ya kutambua vitendo vya ukatili,kuviripoti na kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria". Amesema

Wadau walioshiriki mkutano huo ni pamoja na Wabunge wanawake,wawakilishi wa UNESCO Makao Makuu, na UNESCO Dar es salaam wawakilishi kutoka Habari Maelezo, IPU,TAMWA,Wabunge wanawake kutoka Ghana,Kenya,Uganda na Malawi.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger