Monday 18 September 2023

MKURUGENZI MANISPAA YA TABORA AMPA SIKU TATU MKUU WA KITENGO CHA TAKA NGUMU KUONDOSHA TAKA ZOTE ZILIZOLUNDIKANA MAENEO YA KUKUSANYIA TAKA

...


Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Ndugu Elias M. Kayandabila amemtaka Mkuu wa Kitengo cha Taka Ngumu Ndugu Adamu Baleche kuhakikisha kuwa ndani ya siku tatu awe ameondosha taka zote zilizopo maeneo yote ya kukusanyia taka na kuzipeleka dampo.

Kanyandabila ameyatoa maelekezo hayo leo Septemba 18, 2023 wakati wa Ziara fupi ya Timu ya Menejimenti ya Halmashauri (CMT) ya kukagua hali ya usafi katika viunga vya Manispaa ya Tabora.

Aidha Ndugu Kayandabila ameunda timu ndogo itakayoshirikiana na Kitengo cha Taka Ngumu katika kuratibu na kusimamia kazi zote za usafi mjini hapo, lengo kubwa ikiwa ni kuongeza ufanisi wa shughuli za usafi katika Manispaa yetu.

Wajumbe wa CMT nao baada ya kujionea hali mbaya katika maeneo ya kukusanyia taka, wameafiki kwa pamoja umuhimu wa timu hiyo ndogo ambayo itaongeza nguvu kwenye kitengo cha taka ngumu.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger