Thursday 21 September 2023

MWANAMKE ATUPWA JELA BAADA YA KUPOST VIDEO TIKTOK AKILA KITIMOTO

...
Mahakama ya Indonesia imemfunga jela mwanamke mmoja miaka miwili baada ya kupatikana na hatia ya kukiuka sheria za kukufuru za nchi hiyo katika video ya chakula ya TikTok aliyochapisha mwezi Machi.

Video hiyo ilionyesha Lina Lutfiawati akisoma sala ya Waislamu kabla ya kula ngozi ya nyama ya nguruwe iliyokauka na kukusanya mamilioni ya watu waliotazama .

Nyama ya nguruwe inachukuliwa kuwa 'haram', au hairuhusiwi, chini ya sheria za Kiislamu.

Siku ya Jumanne, mahakama katika mji wa Palembang nchini Indonesia, sehemu ya kusini ya kisiwa cha Sumatra, ilimpata kijana huyo mwenye umri wa miaka 33 kwa hatia ya "Kueneza habari zilizokusudiwa kuchochea chuki au uadui wa mtu binafsi/kikundi kwa misingi ya dini" na kumuamuru kulipa faini ya rupiah milioni 250 ($16,249.59).

Indonesia ni taifa kubwa zaidi duniani lenye Waislamu wengi.

Mahakama ilisema Lutfiawati, ambaye pia anafahamika kwa jina Lina Mukherjee, aliyetambulika kama Muislamu.

Lutfiawati aliomba radhi kwa umma kwa video hiyo na kueleza kushangazwa na hukumu hiyo.

"Ninajua kuwa nina makosa, lakini sikutarajia adhabu hii," Lutfiawati alisema kwenye kituo cha habari cha MetroTV.

Kesi hiyo ni ya hivi punde zaidi kati ya kesi kadhaa za kashfa kote nchini, haswa dhidi ya zile zinazodaiwa kuutusi Uislamu, ambazo wachambuzi wamesema zinadhoofisha sifa ya Indonesia ya kuwa na msimamo wa wastani.

Mnamo Agosti, mkuu wa shule ya bweni ya Kiislamu ambayo iliruhusu wanaume na wanawake kusali pamoja na wanawake kuwa wahubiri alishtakiwa kwa kukufuru na matamshi ya chuki.

CHANZO - BBC SWAHILI
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger