Saturday 28 September 2019

ZESCO UNITED WAICHAPA YANGA 2-1 , LIGI YA MABINGWA AFRIKA

...
Na mpiira, umekwisha, Yanga inaondolewa rasmi kwenye mashindano ambapo itacheza Shirikisho na Zesco inaingia hatua ya makundi.

Dak ya 90+4, Zesco wanacheza kwa akili ya kumaliza dakika zilizoongezwa.
Dak ya 90, Moro anapewa kadi nyekundu kwa kucheza madhambi, sasa Yanag wamebaki pungufu. Dakika nne za nyongezwa zinaoneshwa na Mwamuzi wa mezani.

Dak ya 85, Kamusoko anapiga faulo, inaokolewa.
Dak ya 84, faulo nyingine karibu kabisa na eneo la hatari mwa Yanga inapigwa na Zesco. Kamusoko anaonekana na mpira. Muda huo Ally Ally anatoka na Kalengo anaingia kuchukua nafasi yake.
Dak ya 83, Maybin Kalengo anaokena akiandaliwa, bila shaka anataka kuingizwa kuchukua nafasi ya mtu mwingine.
Dak ya 82, hali inakuwa ngumu sasa kwa Yanga, wanapaswa kusawazisha ili mechi iongezwe dakika 30 za ziada.

Dak ya 78, Makame anaizawadia Zesco bao la pili kwa kujifunga, sasa ni 2-1.
Dak ya 69, Yanga wanakosa utulivu wa kutengeneza bao la pili, ni baada ya krosi safi kupigwa engo ya kushoto mwa uwanja lakini inakosa wa kuifanyia kazi.
Dak ya 69, kina nyingine kwa Zesco kipindi hiki cha pili, inapigwa na inaokolewa.
Dak ya 63, Metacha anaanza tena upya.
Dak ya 62, hatari nyingine inatokea katika lango la Yanga, mipira yao ya vichwa inashindwa kufanya walichodhamiria. 

Dak ya 59, Zesco wamekuwa wakifanya mashambulizi mengi japo yamekuwa yakikosa utulivu na ubora wa Yanga eneo la ulizi unakuwa vizuri.
Dak ya 56, Faulo nyingine inapigwa kuelekezwa Yanga, pigwa pale Yanga wanaokoa, unatanguliwa mbele kwake Sadney, unamkuta kipa Banda, anaanza upya.
Dak ya 54, faulo inapigwa na Yanga wanaokoa, wakati huo mchezaji mmoja wa Yanga ameodondoka.
Dak ya 54, Kelvin Yondani anapewa kadi ya njano kwa kucheza madhambi, inakuwa kadi ya nne katika mchezo huu, Yanga wana tatu na Zesco moja.

Dak ya 51, Zesco sasa wanamiliki, mpira anakwenda kwake Kamusoko, hatari kule, Yanga wanaokoa, ilikuwa hatari aisee.
Dak ya 49, Yanga wanafanya shambulizi jingine lango ni mwa Zesco lakini linashindwa kuzaa matunda.
Dak ya 49, Ally Ally anarusha mpira kuelekea Zesco baada ya kutolewa nje.
Dak ya 48, mpira upo kwake Mnata hivi sasa, anaanzisha upya.
Dakika 45 za kipindi cha pili kimeanza

MAPUMZIKO: ZESCO 1-1 YANGA

Dak ya 43, Zesco wanapata faulo karibu kabisa na eneo la penati, ni baada ya Ally Ally kucheza sivyo, wakati huo kuna mchezaji wa Yanga ameanguka chini.
Dak ya 42, Zesco wanajaribu kusaka lango la Yanga kwa nguvu lakini mabeki wake wanapambana kuwazuia, wameongeza kasi.
Dak ya 41, Mpira unarushwa kuelekezwa Yanga.

Dak ya 39, Yanga wanapata kona, inapigwa lakini inashindwa kuzaa matunda.
Dak ya 37, ni faulo, kadi nyingine na ya pili kwa Yanga inenda kwa Moro baada ya kucheza madhambi.
Dak ya 35, Zesco wnafanya shambulizi jingine, Kamusoko anao mpira, Yanga wanaokoa.
Dak ya 34, Yondani anafanyiwa faulo na mpira unapigwa kuelekea Zesco United.
Dak ya 30, Yanga wanakosa nafasi nyingine, inakuwa kona, anakwenda kupiga Sibomana, kwake Sadneeeey, gooli, wanasawazisha.

Dak ya 27, Kaseka anapata kadi ya njano kwa kucheza madhambi, ni kadi ya kwanza kwa dakika 45 za kwanza.
Dak ya 24, Goooli, Zesco wanapata bao la kwanza kupitia kwa Jesse Were akifunga kwa kichwa.
Dak ya 22, Zesco wanazidi kutawala, mpira unarushwa kuelekezwa langoni kwao.
Dak ya 21, Zesco wanaonekana kutawala eneo la kati, wakipambana kusaka namna ya kuipenya ngome ya Yanga.
Dak ya 20, Zesco wanarusha mpira kuelekea Yanga, ni faulo tena Akumu anachezewa, hapana ni offside, Yanga wanacheza.

Dak ya 19, Kamusoko anapiga lakini mabeki wa Yanga wanaokoa.
Dak ya 18, Zesco wanapata faulo, anaenda kupiga Kamusoko, ni kushoto kidogo, mita chache karibu na eneo la hatari.
Dak ya 16, Kaseke anapasiana na Ally Ally kulia kwenye kona ya kulia mwa kibendera lilipo lango la Zesco lakini wanashindwa kuwa watulivu na wapinzani wanauchukua.
Dak ya 14, mlinda mlango wa Zesco Jacob Banda anaonekana akituliza mpira kwa madaha, ni dalili za kupoteza muda ikiwa ni dakika za mapema.
Dak ya 12, Levy Mwanawasa hakuna watu, idadi ndogo ya mashabiki inaonekana.

Dak ya 11, Sadney Urikhob anatoa mpira nje ambao kama angeutuliza vizuri ungeweza kuwa na faida kwa Yanga.
Dak ya 10, ni goli-kiki, kipa Mtacha anonekana akiwaambia jambo wachezaji wake.
Dak ya 09, Tshishimbi anatoa mpira nje, unarushwa kuelekezwa Yanga.
Dak ya 09, Yanga wanafanya shambulizi kali lakini umakini wa kumalizia kambani unakosekana.
Dak ya 08, bado mchezo haujawaa na utulivu kwa timu zote mbili.

Dak ya 07, kona nyingine wanapata Zesco united, wanapiga na Yanga wanaokoa, Lamine Moro anapiga kichwa.
Dak ya 06, Zesco wanapata kona ya kwanza.
Dak ya 05, Tshishimbi anapata nafasi ya kutengeneza shambulizi lakini mabeki wa Zesco wanakuwa mahiri, wanamzuia.
Dak ya 04, faulo inapigwa kuelekezwa katika lango la Yanga.
Dakika 45 za kwanza zimeanza katika uwanja wa Levy Mwanawasa, Ndola, Zambia.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger