Monday 1 April 2019

WADAU WAKUTANA KUJADILI CHANGAMOTO KWENYE TASNIA YA HABARI TANZANIA

...

Picha ya pamoja ya washiriki wa semina hiyo

MISA Tanzania na shirika linalojikita katika kuimarisha uwezo wa vyombo vya habari ili kupunguza migogoro, kuimarisha demokrasia na kuwezesha uhuru wa kupata taarifa la IMS zimewakutanisha wadau mbali mbali katika semina ya kujadili mazingira yaliyopo na kupendekeza namna ya kuzikabili changamoto zinazodumaza sekta ya habari na uhuru wa kujieleza nchini.

Semina hiyo ya siku mbili iliyofanyika mwishoni mwa wiki mkoani Morogoro iliwakutanisha wawakilishi wa wadau mbalimbali wa tasnia ya habari ikiwemo waandishi wa habari,asasi za kiraia,wanasheria pamoja na wahadhiri wa vyuo vikuu.

Wakijadili,walitaja baadhi ya changamoto zikiwemo za kiuchumi miongoni mwa wanahabari,sheria zisizo rafiki,wadau kutokuwa na uelewa mzuri wa sheria na kanuni washiriki hao wamesema kuwa kutokuwa na umoja thabiti na nia ya pamoja ndio imekuwa chanzo kikuu cha matatizo mengine kunawiri na kupendekeza kuwa kabla ya kutafuta suluhu nyingine,mkazo uwekwe katika kuwa na umoja thabiti na nia ya pamoja miongoni mwa wadau wote wa tasnia ya habari.
Bw.Rashweat kutoka International Media Support (IMS) akielezea umuhimu wa ushirikishwaji kwa kila mdau katika mchakato wa kukuza sekta ya habari na uhuru wa kujieleza.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Bw.Alex Benson (wa kwanza kushoto aliyeketi) akielezea umuhimu wa wanahabari kuwa na uelewa wa kanuni zinazowasimamia ili kuepuka kuzikiuka mara kwa mara.
Wakili James Marenga akiwasilisha mada kwa niaba ya kundi la majadiliano katika semina hiyo
Dr.Geofrey Chambua mshauri wa maendeleo na sheria akielezea uzoefu wake katika kushirikiana na wadau wa sekta mbalimbali kutatua changamoto za kimaendeleo.
Mwandishi wa habari wa kujitegemea kutoka Zanzibar Bw.Ali Othman akichangia mawazo katika semina hiyo
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha St.John (SMC) Bw.Michael Gwimile akichangia mada katika semina hiyo
Bi.Joyce Shebe mhariri Clouds Media akiwasilisha mada kwa niaba ya kundi la majadiliano katika semina hiyo.
Kaimu mkurugenzi wa MISA Tanzania Gasirigwa Sengiyumva akitoa neno la shukrani na kuhitimisha semina hiyo.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger