Thursday, 18 April 2019

Jeshi Lililompindua Rais Omar Al- Bashir Latoa Maagizo Kwa Benki Kuu Ya Sudan

...
Baraza la Kijeshi linaloongoza serikali ya mpito nchini Sudan limeiamuru Benki Kuu ya nchi hiyo, kuchunguza shughuli zote za uhamishaji wa fedha zilizofanyika kuanzia Aprili 1, na kushikilia fedha zote zinazotiliwa shaka. Hayo yameripotiwa leo na shirika la habari la Sudan, SUNA. 

Baraza hilo pia limeamuru kusimamishwa kwa shughuli ya kubadilishwa umiliki wa hisa, hadi itakapotangazwa vinginevyo. 

Benki Kuu vile vile imeamuliwa kuripoti kwa mamlaka husika, juu ya kufanyika mchakato wowote wa uhamishaji mkubwa, au unaotiliwa shaka ya hisa pamoja na umiliki wa makampuni.


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger