Tuesday, 23 April 2019

BABA AMBAKA MTOTO WAKE MKESHA WA PASAKA

...

Mkazi wa Kijiji cha Nyantorotolo Kata ya Nyankumbu Halmashauri ya Mji wa Geita, Patrick Andrew (41) anashikiliwa na Polisi Mkoa wa Geita kwa tuhuma za kumbaka mtoto wake wa kufikia wa miaka 7, ambaye ni mwanafunzi wa darasa la pili.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo amesema kwa sasa jina la mtoto huyo wanalihifadhi, lakini alikuwa akisoma Shule ya Msingi Nyankumbu, ambapo ameeleza mwanamume huyo alifanya kitendo hicho majira ya saa tano usiku siku ya mkesha wa Pasaka

Aidha Kamanda Mponjoli amesema mtu pekee ambaye aligundua mtoto kufanyiwa vitendo hivyo vya kinyama ni mama mzazi wa mtoto huyo, ambaye pia alibainisha kulihifadhi jina lake.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger