Hatimaye Serikali ya CCM chini ya uongozi wa Mh Rais Dr John Pombe Joseph Magufuli imesikia kilio cha wakulima wa Zabibu mkoani Dodoma cha ukosefu wa soko la zabibu kutokana na tozo kubwa ya ushuru wa bidhaa iliyokuwa ikitozwa Tsh 3,315 kwa lita kwa kinywaji kikali kitokanacho na mchuzi wa zabibu. Akichangia leo Bungeni katika Muswada wa Marekebisho ya Sheria Na.2/2019 Mbunge wa Viti Maalum Mh Mariam Ditopile ameishukuru serikali kwa kuleta mabadiliko hayo ya ushuru wa bidhaa na kupunguza tozo hiyo ambayo itawasaidia wakulima kupata soko la uhakika wa…
0 comments:
Post a Comment