Friday, 8 February 2019

Breaking News : HIACE YAGONGANA NA LORI KISHA KUWAKA MOTO MLIMA NYANGOYE BUKOBA, KUNA TAARIFA YA VIFO

...

Watu kadhaa wanahofiwa kupoteza maisha katika ajali  iliyohusisha magari aina ya Canter lenye namba za usajili T223ATK na Hiace yenye namba za usajili T869 GHT kugongana  katika Mlima Nyangoye  eneo la Hamugembe Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.

Ajali hiyo imetokea usiku huu Februari 8,2019

Taarifa za awali kutoka eneo la tukio zinasema kuna taarifa ya vifo vya abiria,idadi haijulikani na bado mamlaka husika hazijazungumzia tukio hilo.

Malunde1 blog inaelezwa kuwa Hiace /daladala yenye Jina la Kitunze Kidumu inayofanya safari zake Bukoba - Mtukula ilikuwa inaelekea kupaki.

Taarifa Kamili tutawaletea hapa Malunde1 blog

Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger