Friday 3 December 2021

JAMBAZI AJISALIMISHA POLISI...AAHIDI KUWA RAIA MWEMA

...



Mwanaume mmoja, Faida Komanya (34) mkazi wa Kijiji cha Bugalagala Wilaya ya Mbogwe mkoani Geita ambaye alikuwa akituhumiwa na Jeshi la Polisi kwa kujihusisha na vitendo vya ujambazi, amejisalimisha kwa jeshi hilo na kuomba apelekewe kama raia mwema baada ya kujirekebisha tabia.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe, amesema mwanaume huyo amehusika katika matukio mengi ya kijambazi na aliwahi kufungwa katika Gereza la Butimba, Mwanza.

Kamanda Mwaibambe ameongeza kuwa kwa mujibu wa Komanya, ameamua kujisalimisha baada ya kupoteza ndugu wengi kwa kuuawa pamoja na kutengwa na ndugu wengine pamoja na jamii.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger