Saturday 18 December 2021

ASKARI POLISI ALIYESIFIA POMBE 'Gongo' AFUKUZWA KAZI

...



Konstebo wa Polisi, Ramadhani Khalfan Said amefukuzwa kazi kwa kwenda kinyume na mwenendo mema wa Jeshi la Polisi Tanzania baada ya kunaswa kwenye mkanda wa video akisifia pombe haramu aina ya gongo huku akiwa amevalia sare za jeshi hilo.

Imeelezwa kuwa kitendo hicho cha askari huyo aliyekuwa na namba G2308 kimelifedhehesha Jeshi la Polisi baada ya video hiyo kusambaa mitandaoni akisema kwamba Gongo ni pombe safi akiipa jina la NIPA (New International Pure Alcohol), video ambayo imeonwa na watu wengi akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger