Friday 3 December 2021

NSSF YATUNUKIWA TUZO KUTHAMINI MCHANGO WAKE KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

...

Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Ekwabi Mujungu (kushoto), ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, akipokea tuzo na cheti kutoka kwa Mgeni Rasmi, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, kwa ajili ya kuthamini mchango wa NSSF katika mapambano dhidi ya UKIMWI. Tuzo hiyo ilitolewa wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani yaliyofanyika kitaifa katika viwanja vya Ruanda Nzovwe mkoani Mbeya. Katikati ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS Dkt. Leonard Maboko.
Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala (NSSF), Ekwabi Mujungu (wa tatu kulia) ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa NSSF baada ya kupokea tuzo na cheti kwa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kuthamini mchango katika katika mapambano dhidi ya UKIMWI. Wa tatu kushoto ni Meneja wa NSSF Mkoa wa Mbeya, Deus Jandwa.
Tuzo na cheti kutoka TACAIDS cha kuthamini mchango wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika mapambano dhidi ya UKIMWI
HUDUMA: Wananchi walipokuwa wanahudumiwa kwenye banda la NSSF wakati wa maonesho ya Maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani yenye kauli mbiu 'Zingatia usawa. Tokomeza UKIMWI. Tokomeza Magonjwa ya Mlipuko ' , yanayofanyika kitaifa Mkoani Mbeya, ambapo Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) unashiriki kutekeleza Sera ya Utumishi wa Umma kuhamasisha elimu juu ya VVU, UKIMWI na magonjwa sugu yasiyoambukizwa mahala pa kazi
Katibu Mahsusi ambaye pia Mwelimishaji rika wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii(NSSF) Mkoa wa Mbeya, Happy Gwimile (wa kwanza Kulia) akiwakumbusha baadhi ya wananchi waliotembelea banda la NSSF kuhusu kuendelea kujikinga na maambukizi VVU na UKIMWI hasa mahali pa kazi ili kulinda nguvu kazi ya Taifa.
Afisa Mkuu Utawala Daniel Shaidi (kushoto) wa NSSF Makao Makuu ambaye pia ni Mwelimishaji rika mahala pa kazi, alipokuwa anamuelekeza Fatma Fungo (kulia), namna ya kutumia mifumo mbalimbali inayomwezesha mwanachama kuangalia taarifa zake kupitia simu ya kiganjani bila kulazimika kufika katika Ofisi za NSSF. Mifumo hii ni pamoja na NSSF Taarifa , Whatsapp na ujumbe mfupi wa maneno yaani SMS. Mifumo hii ya kidigitali inamrahisishia mwanachama kupata huduma kwa haraka kwa kujihudumia mwenyewe, inampunguzia gharama za usafiri. Maonesho ya Maadhimisho ya siku ya UKIMWI duaniani Kitaifa yanafanyika katika Mkoa wa Mbeya.
Katibu Mahsusi ambaye pia Mwelimishaji rika wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii(NSSF), Ng’walu Mihambo kutoka NSSF Tarime, akitoa maelezo kwa wananchi juu ya mbinu za kuzuia magonjwa ya VVU, UKIMWI na magonjwa sugu yasiyoambukiza ikiwa ni pamoja na ulaji unaofaa, mazoezi ya mwili, kuwa na uzito usiozidi kiasi kulingana urefu, kuepuka matumizi ya pombe na sigara, VVU, UKIMWI na magonjwa sugu yasiyo ambukizwa
Afisa Mwandamizi Utawala, Naphisa Jahazi ambaye pia ni Mwelimishaji rika mahala pa kazi kutoka NSSF, Mkoa wa Temeke akielezea kwa baadhi ya wananchi namna NSSF ilivyojielekeza katika kudhibiti VVU, UKIMWI na magonjwa sugu yasiyoambukizwa mahala pa kazi, wakati wa Maonesho ya Maadhimisho ya siku ya UKIMWI duaniani Kitaifa yanafanyika katika Mkoa wa Mbeya
Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), haujawaacha nyuma makundi yenye mahitaji maalum, Mkalimani wa Lugha ya alama Baraka Bakari (wa kwanza kulia) akiwatafsiria walemavu wa usikivu elimu kuhusu hifadhi ya jamii, walipotembelea banda la NSSF wakati wa Maonesho ya Maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ambayo Kitaifa yamefanyika Mbeya
  *****

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umepewa tuzo kama ishara ya kuthamini mchango wake katika mapambano ya VVU na UKIMWI.


Tuzo hiyo ilitolewa na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na kukabidhiwa na mgeni rasmi ambaye ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, wakati wa maadhimisho ya siku ya UKiMWI duniani yaliyofanyika jijini Mbeya.


NSSF imekuwa ikitekeleza Sera ya UKIMWI mahala pa kazi na imekuwa ikisimamia miongozo yote inayohusu VVU na UKIMWI


Pia, Mfuko ulishiriki katika maonesho na maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ili kuendelea kutoa elimu kuhusu umuhimu wa Taifa kuendelea kujikinga na masuala ya VVU na UKIMWI.


Mkurugenzi Mkuu Bw. Masha J. Mshomba katika salamu zake kwa wafanyakazi wa Mfuko katika siku ya UKIMWI duniani alisema “Nasisitiza kuwa, ni wajibu wa kila mfanyakazi kuchukua hatua katika kudhibiti VVU na UKIMWI ili kuokoa nguvu kazi ya Mfuko na Taifa”.


Aidha, Mshomba alifafanua zaidi na kusema kwamba NSSF inayo sera inayohusu masuala ya VVU na UKIMWI ambayo inasisitiza kujilinda, kujikinga, kumlinda mfanyakazi aliyeathirika, kuzuia unyanyapaa na kumsaidia mfanyakazi aliyeathirika.
Kauli Mbiu ya mwaka huu ilikuwa “Zingatia Usawa, Tokomeza Ukimwi, Tokomeza Magonjwa ya Mlipuko”.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger