Wednesday 5 August 2020

ACT WAZALENDO YASISITIZA KAZI NA BATA...VYAMA VYA SIASA VYAKUMBUSHWA KUFUATA SHERIA

...
Kiongozi wa Chama Cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe 

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kiongozi wa Chama Cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amesema vyama vya upinzani nchini Tanzania vimejipanga kikamilifu kuhakikisha vinapata ushindi mkubwa katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28,2020.

Zitto Kabwe ameyasema hayo leo kwenye Mkutano Mkuu  wa ACT Wazalendo Taifa unaofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.

"Sisi kama vyama vya upinzani tutaweka wagombea makini kuanzia ngazi ya Rais,Madiwani na Wabunge. Tutahakikisha tunashinda kwenye uchaguzi Mkuu 2020",amesema.

"Tutaendelea kufanya juhudi hadi za dakika za mwisho kuweka ushirikiano ili kupata ushindi katika uchaguzi.Vyama vya UpinzaniaTutakuwa wamoja,Inawezakana kufanya kazi huku tukila bata. Tunaamini katika Kazi na Bata",amesema Zitto Kabwe.

Naye Mwakilishi wa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Sisty Nyahoza amevitaka vyama vya siasa nchini kufuata sheria katika uchaguzi mkuu 2020.

"Mhe. Mwenyekiti fanyeni mbwembwe zote,propaganda zote kwa mujibu wa sheria. Hamuwezi kila chama mkafikia malengo yenu bila kufuata sheria. Tunawaasa uchaguzi uende kwa mujibu wa sheria",amesema Sisty.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger