Monday 2 January 2017

Tulia: Tanzania mpya inawezekana

...

Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson amesema kuwa Tanzania mpya yenye matokeo chanya kwa mwaka 2017 iwapo inawezekana  iwapo kila mmoja wetu atafanya kazi kwa bidii ili kuliletea taifa maendeleo.

Ameyasema hayo wakati wa ibaada maalum  ya mkesha wa kitaifa wa mwaka mpya uliofanyika katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam, Dk. Tulia amewataka watanzania kuwa na ushirikiano wa pamoja ili kufikia maendeleo.

“Tanzania mpya na nchi mpya yenye matokeo chanya kwa mwaka 2017 inawezekana hivyo tushirikiane kwa pamoja na kila mmoja akifanya kazi kwa bidii, lazima maendeleo yatapatikana tu”amesema Dk. Tulia.

Aidha, amewataka watanzania kuendelea kutoa ushirikiano kwa viongozi wa serikali ili waweze kupata maendeleo kwa haraka zaidi.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger